June 13, 2015

EMIRY (MBELE), SIMBA IKO KATIKA HATUA ZA MWISHO KUMSAJILI.
Kamati ya Usajili ya Simba iko katika hatua ya mwisho kumsajili beki wa pembeni, Nimubona Emiry ambaye ni kiboko.

Emiry ana uwezo wa kucheza kwa ustadi mkubwa beki zote mbili za kulia na kushoto ambazo Simba zaidi wanawategemea Ramadhani Kessy na Mohammed Hussein ‘Tshabalala’.

Emiry raia wa Burundi bado yuko Vital’O ya Burundi na tayari Simba imeanza mazungumzo naye ambayo yamefika katika nzuri.


Iwapo watakubaliana, kiongozi mmoja wa Simba anaweza kukwea pipa na kwenda kumsajili beki huyo anayeaminika ataleta upinzani mkubwa kwa mabeki wa pembeni wa Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic