June 24, 2015


Pamoja na kufanya jitihada za kumnasa mshambuliaji Laudit Mavugo, Simba bado inadaiwa na Vital’O ya Burundi na imekiri.


Vital’O inaidai Simba dola 5,000 (zaidi ya Sh milioni 10) ikiwa ni sehemu ya fungu la usajili wa Amissi Tambwe.

Tayari Tambwe yuko Yanga baada ya Simba kumtema, lakini bado hawajalipwa fedha hizo.

Taarifa za awali zilieleza kuwa deni hilo limevuruga hata usajili wa Mavugo kwa Vital’O kutaka kulipwa kwanza fedha za Tambwe.

Lakini uongozi wa Simba kupitia mjumbe wake wa kamati ya utendaji, Collins Frisch ikatoa ufafanuzi kwamba la hasha.

“Hakika hilo deni lipo na tumelikubali hata kama lilikuwa wakati wa uongozi uliopita, lakini Simba ndiyo hii,” alisema Frisch.


“Lakini tumeelewana vizuri na Vital’O na tuko katika mchakato wa kulipa lakini hilo halijaingiliana na usajili wa Mavugo, si kweli.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic