July 3, 2015

GARI LA TAMBWE....
Straika wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe, juzi Jumatano alipata ajali baada ya gari lake aina ya Toyota Mark X kugongwa na Bajaj katika eneo la Tandale kwa Mtogole wakati akielekea mazoezini.


Tambwe ambaye ni mfungaji bora wa msimu wa 2013-2014, amesema ajali hiyo ilitokea baada ya dereva wa Bajaj kutaka kulazimisha kupita sehemu ambayo hakutakiwa kupita kwa mujibu wa sheria za barabarani.
    
TAMBWE WAKATI WAKIWA SIMBA“Nimepata ajali asubuhi wakati nakuja mazoezini pale katika eneo la Tandale kwa Mtogole, kuna Bajaj ilitokea kwa nyuma yangu, sasa dereva akalazimisha kupita katika upande wangu na njia ilikuwa ndogo, gari imeumia kwa sababu amechuna rangi na ameng’oa bampa la mbele.


“Nilimsamehe palepale kwa sababu sehemu iliyoharibika haikuwa kubwa ila kama angevunja taa tungekamatana ila nitaipeleka gereji kwa ajiili ya matengenezo na ipakwe rangi ili iwe na muonekano wa awali,” alisema Tambwe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic