July 3, 2015


Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Geofrey Mwashiuya, ameonekana kuendelea kuandamwa na majanga muda mfupi baada ya kuanza kuitumikia Yanga.


Ikiwa ni siku chache tangu kuripotiwa kuwa klabu yake ya zamani ya Kimondo ya Mbeya ipo tayari kupinga yeye kucheza Yanga, kiungo huyo amepata majeraha ya goti ambayo yatamweka nje kwa siku kadhaa.

Mwashiuya ambaye ameonyesha uwezo wa juu katika muda huo mfupi aliokuwa klabuni hapo, alipatwa na balaa hilo baada ya kugongana na beki wa kushoto wa kikosi hicho, Edward Charles.

Daktari wa Yanga, Juma Sufian, amesema kiungo huyo wa pembeni atakuwa nje ya uwanja kwa siku kadhaa akiuguza mguu wake huo.

“Mwashiuya leo (jana) ameshindwa kufanya mazoezi na wenzake kutokana na kuumia goti jana (juzi) mazoezini na sasa anaendelea na tiba.

“Ni matumaini yetu kuwa, baada ya siku tatu anaweza kurejea uwanjani kuendelea na mazoezi kwa sababu maendeleo yake siyo mabaya sana,” alisema Sufian.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic