July 8, 2015


Kikosi cha Mbeya City kinatarajiwa kuanza kujiwinda rasmi kwa ajili ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara na kimepanga kutumia siku 32.


Ligi inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 22, mwaka huu katika viwanja tofauti hapa nchini.

Msimu uliopita, Mbeya City ilifanikiwa kumaliza nafasi ya nne licha ya kuanza ligi kwa kusuasua   chini ya kocha wake mkuu Juma Mwambusi na imefanikiwa kusajili wachezaji watatu huku  wachezaji kumi wakiondoka.

 Katibu wa timu hiyo, Emmanuel Kimbe, alisema wanatarajia kuanza maandalizi yao na wataingia kambini Julai 20, mwaka huu.

“Wachezaji  wanatarajiwa  kuingia kambini na kujiwinda mapema Julai 20, mwaka huu na lengo ni kuhakikisha tunafanya vizuri na huku ndiko mwalimu ataweza kuainisha mipango yake na hata kuweza kuangalia michezo ya kirafiki ili kujiweka imara zaidi.


“Kwa sasa hivi tumesajili wachezaji watatu,  kama kutakuwa na uhitaji mwingine, tutaweza kuongeza wachezaji ingawa kila nafasi  sasa hivi ipo vizuri,” alisema Kimbe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic