July 4, 2015


Miaka mitatu sasa, Simba haijafuzu kushiriki michuano ya kimataifa inayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf), hiyo haimsumbui straika mpya aliyerejea kikosini, Mussa Mgosi ambaye amewataka mashabiki kutulia kwani hali hiyo itarejea ndani ya msimu huu.


Mgosi aliyejiunga na Simba siku chache zilizopita baada ya kumaliza mkataba na Mtibwa Sugar, amesema: “Heshima iliyopotea Simba, sasa itarudi.”

Alisema kwa kushirikiana na wenzake, atahakikisha msimu ujao watafanya kila liwezekanalo ili Simba kama siyo kutwaa ubingwa basi ishike nafasi ya pili na kukata tiketi ya kucheza michuano ya Caf.

“Nimetoa kauli hiyo kwa kuzingatia usajili uliofanywa kwa maana wale tunaojiunga na timu tukishirikiana na wenzetu tuliowakuta hapo tutakuwa na timu bora,” alisema Mgosi.

 “Sasa ndiyo muda wa Simba kurudisha heshima yake kama zamani kwani imedharaulika kwa muda mrefu lakini napenda kusema msimu uliopita ndiyo ulikuwa mwisho wa dharau hizo.”

Mbali na Mgosi, wachezaji wengine waliosajiliwa na Simba hadi sasa ni kiungo Peter Mwalyanzi kutoka Mbeya City, Mohammed Fakhi (KMKM), Samih Ali Nuhu (Azam FC), Laudit Mavugo na Nimubona Emiry (Vital’O) na kiungo Emmanuel Ntinde kutoka Burkina Faso ya Morogoro.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic