July 8, 2015


Mambo yanaonekana kuanza kumnyoookea mshambuliaji wa Simba, Alex Masawe, ambaye anafanya majaribio na kikosi hicho akitokea timu ya Olympic ya Afrika Kusini inayoshiriki Ligi Daraja la Pili.


Mshambuliaji huyo mwenye mwili uliojengeka kimazoezi, amejiunga na kikosi cha Simba tangu siku ya kwanza katika programu ya gym, huku pia akijumuishwa katika kikosi kilichosafiri kuelekea Tanga kwa ajili ya kujiandaa na ligi kuu.

Kocha msaidizi wa timu hiyo, Selemani Matola, amesema mchezaji huyo ana nidhamu pia anaonyesha juhudi kubwa katika mazoezi, lakini watautathimini uwezo wake zaidi katika michezo ya kirafiki wanayotarajia kucheza hivi karibuni.

“Huyu ni kijana mzuri kwa sababu ana nidhamu nzuri na anaonyesha juhudi kubwa katika programu zetu tukiwa gym na beach. Kama akiendelea hivi, anaweza kuwa katika nafasi nzuri ya kufuzu majaribio yake.

“Siwezi kusema amefuzu moja kwa moja, bado tunahitaji kumuangalia katika mechi. Kwa hiyo michezo michache ambayo tumepanga kucheza katika siku za hivi karibuni, ndiyo itakayotoa jibu kamili juu ya hilo,” alisema Matola.

Kwa upande wake, Massawe alisema:


“Ninafurahia programu jinsi zinavyokwenda, kila siku unapata kitu kipya. Ninaamini nimefanya kwa ubora katika mazoezi yetu ya kila siku. Suala la kupata mkataba linabaki mikononi mwa makocha kwa sababu wao ndiyo wanajua umuhimu wangu katika timu,” alisema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic