Na Saleh Ally
MAPEMA kabisa, utamu wa michuano ya Kombe la Kagame umeanza kuonekana. Tumeanza kuona kwamba hata timu zilizoonekana hazitafanya lolote, zinaweza kuwa na upinzani mkubwa.
MAPEMA kabisa, utamu wa michuano ya Kombe la Kagame umeanza kuonekana. Tumeanza kuona kwamba hata timu zilizoonekana hazitafanya lolote, zinaweza kuwa na upinzani mkubwa.
KMKM
walioonekana hawatakuwa na lolote, wameanza na ushindi, Yanga walioonekana
wataitandika kila timu, wameanza na kipigo.
Al
Shandy ya Sudan ambayo ilionyesha soka safi na la kuvutia, imeishia kupokea kipigo
katika mechi yake ya kwanza dhidi ya APR ya Rwanda ambayo katika mechi ya
kwanza, haikuwa katika kiwango chake cha juu kama timu, isipokuwa wachezaji
kuonyesha uwezo wao binafsi.
Kila
kitu kimeanza tofauti na ilivyokuwa ikionekana itakuwa kabla haijaanza. Huo
ndiyo mchezo wa soka, ndiyo maana unapendwa kuliko mwingine wowote kwa kuwa
hauna majibu au matokeo mgando. Yanabadilika wakati wowote.
Wakati michuano hiyo inaendelea, kila mchezaji
angependa kujiuza kwa maana ya kupata soko zaidi, iwe katika timu zinazoshiriki
michuano hiyo au nje ya hapo.
Juhudi katika kazi, maana yake upate
mafanikio. Mafanikio maana yake ni kupata maslahi zaidi. Runinga maarufu ya
masuala ya michezo barani Afrika, inaonyesha michuano hiyo moja kwa moja.
Kabla sijaelezea faida zake, kidogo ngoja
nieleze haya kuhusiana na watangazaji wengi wa runinga hiyo ambayo naona ina
faida kubwa ya kuwauza wachezaji wa ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuwa
inaonekana katika eneo kubwa la Bara la Afrika na kwingineko duniani.
Asilimia kubwa ya watangazaji wake, hata watu
wanaoshika kamera wanatokea nchini Kenya. Sasa kiasi fulani walionyesha
ushabiki wa waziwazi wakati Yanga ikipambana na Gor Mahia. Baadhi yao hata
makosa ya wazi ya wachezaji wa timu hiyo ya Kenya, walikaa kimya bila ya
kuyazungumzia, lakini waliyofanya wachezaji wa Yanga, yakazungumziwa.
Nawakumbusha, michuano hii inachezwa
Tanzania. Hapa kuna vyombo vingi vya habari kuliko kwao. Ikiwa ni suala la
kukiuka weledi, basi ubaya utawaangukia wao. Wafuate weledi kwa maana ya
kuusaidia ukanda wetu, ushabiki upungue.
Nikirudi kwenye faida, timu tatu za Tanzania
zinazoshiriki michuano hiyo yaani Yanga, Azam FC na KMKM zina nafasi ya kufanya
vema na pia kupata faida ya wachezaji wake kuonekana.
Hali inavyoonekana, timu za Tanzania ndizo
zinazotaka wachezaji kwa ajili ya kuwasajili kupitia michuano hiyo. Si Jambo
baya, lakini tujiulize, kwani wachezaji wa Tanzania hawataki kusajiliwa Sudan,
Kenya, Rwanda au kwingineko barani Afrika au Ulaya?
Sasa
vipi Watanzania waangalie kununua tu bila ya kuuza? Kama kweli soka ni biashara,
sasa vipi wao wanafanya biashara ya kununua pekee bila ya kuuza kwa faida ili
kuthibitisha soka sasa ni biashara?
SuperSport ina nafasi ya kuwafikishia ujumbe
mawakala katika nchi rundo za Afrika kuhusiana na michuano hiyo. Vizuri kama
juhudi kwa wachezaji 60 kutoka wachezaji wanaocheza katika timu za Tanzania
ikawa ni nguzo kwa maana mbili.
Moja
ni kuzisaidia timu zao kubeba ubingwa, pili ni kukuza soko lao na kupata nafasi
ya kwenda mbali zaidi. Lazima wachezaji wajue, kuwa na wachezaji wengi nje ya
nchi ni sehemu ya maendeleo kisoka.
Kucheza nje ya nchi yako, hata kama itakuwa
jirani ni sehemu ya kujifunza. Inaleta mabadiliko na tabia ya kuwa mshindani.
Hivyo lazima wapambane na kujiuza kwa maana ya kusaka maendeleo zaidi.
Kununua katika michuano hiyo si vibaya, lakini
ili kuonyesha tumepiga hatua kiuchezaji. Basi vizuri pia tukauza tena
ikiwezekana nje ya Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kwa kuwa michuano hiyo
inafuatiliwa.








0 COMMENTS:
Post a Comment