August 31, 2015


Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Haruna Moshi ‘Boban’, anajaribu tena bahati yake ya kucheza soka la kulipwa, baada ya kutimkia nchini Oman kufanya majaribio lakini kuna taarifa nyingine inafafanua kuhusu jinsi Mbeya City ilivyomkosa kiungo huyo dakika za mwisho.


Miaka kadhaa iliyopita, Boban alikuwa akiichezea Gefle IF inayoshiriki Ligi Kuu ya Sweden lakini alishindwa kuelewana na kocha wale, Perre Olson ambaye baadaye alitaka abaki lakini akashindwa kumshawishi Boban ambaye alirejea nchini na baadaye kujiunga na Coastal Union baada ya kukaa msimu mzia bila kucheza.


Inadaiwa kuwa Boban ameshamaliza wiki sasa tangu atimkie zake nchini humo kusaka bahati kwa mara nyingine.

Herry Mzozo ambaye ni kocha wa Friends Rangers ya Ligi Daraja la Kwanza inayommiliki mchezaji huyo, amesema:

 “Boban ameondoka, yupo Oman kwa muda wa wiki sasa. Kuna timu imemuita ambayo itatajwa baada ya kumalizana kila kitu. Mbeya City walionyesha nia ya kumtaka tangu mwanzo lakini sijui ilikuwaje baadaye wakawa kimya.


“Sasa walirejea hivi karibuni kuonyesha kuwa wanamhitaji na wamejikamilisha lakini ikawa wameshachelewa, mipango ya Boban ilikuwa imeshakaa sawa, kwa hiyo wakawa wamepishana naye lakini pengine wangekuwa na maamuzi tangu mwanzo, wangeweza kumchukua,”  alifafanua Mzozo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic