August 14, 2015


Ile ishu ya  Simba kumleta kipa kutoka nchini Brazil, Ricardo Andrade limeyeyuka juu kwa juu sababu kubwa ni uongozi wa timu hiyo kunasa saini ya Muivory Coast, Vincent Agban.


Simba ilikuwa mbioni kumleta nchini Andrade kwa ajili ya kuzungumza naye na kumpa kandarasi kwa ajili ya msimu ujao baada ya kumfanyia majaribio lakini ghafla mpango umegeuka baada ya kuridhishwa na uwezo wa Agban na kumpa mkataba wa miaka miwili.

Awali, Wekundu hao walikuwa na hesabu ya kumuongezea mkataba kipa wao, Ivo Mapunda kisha wamsainishe Mbrazili huyo kwa ajili ya kusaidiana na kipa mwingine kinda, Peter Manyika kwenye Ligi Kuu Bara msimu ujao.

Baada ya kutoelewana na Ivo, ndipo wakaamua kumsainisha Agban na kumtosa Andrade kwa kigezo kuwa haiwezekani nafasi ya kipa ikawa na maprofesheno wawili. Hata hivyo, Rais wa Simba Evans Aveva alisema jana wanatarajia kumalizana na Ivo Mapunda ndani ya siku mbili.

Aidha, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Kassim Dewji, amesema nafasi ya kipa wa tatu, atasajiliwa kipa kutoka Tanzania na tayari wapo sokoni kuangalia atakayewasaidia msimu ujao.

“Agban anatosha, atakuwa na Manyika na watasaidiana na kipa mwingine ambaye tutamsajili kutoka hapahapa Tanzania,” alisema Dewji.


Simba sasa ina wachezaji wa kigeni sita kati ya saba kulingana na kanuni za ligi kuu, wengine ni Waganda, Hamis Kiiza, Juuko Murshid, Simon Sserunkuma, Mzimbabwe, Justice Majabvi na Mrundi, Emiry Nimubona.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic