Kocha Mkuu wa Simba, Dylan Kerr, ametamka kuwa
kati ya nafasi zinazompa changamoto ya upangaji wa timu, basi ni safu ya kiungo
yenye viungo nane.
Safu hiyo ya kiungo inachezwa na Jonas Mkude,
Abdi Banda, Peter Mwalyanzi, Said Ndemla, Mwinyi Kazimoto, Justice Majabvi,
Awadh Juma na Ibrahim Ajibu.
Kocha huyo alitoa kauli hiyo mara baada ya
kumalizika kwa mchezo wa kirafiki dhidi ya SC Villa ya Uganda uliochezwa kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambao ulimalizika kwa Simba kushinda bao
1-0.
Kerr amesema anafurahia kuwa na viungo wote hao
wenye uwezo mkubwa hali inayosababisha apate ugumu wa kupanga kikosi cha
kwanza.
Kerr alisema hana hofu juu ya safu ya kiungo
kutokana na kila mmoja atakayempa nafasi ya kucheza anaonyesha kiwango kikubwa,
tofauti na safu ya ushambuliaji ambayo inahitaji maboresho kidogo.
Aliongeza kuwa, kila kiungo ana nafasi yake ya
kucheza kwenye kikosi chake kutokana na aina ya mechi atakayokutana nayo kwenye
siku husika.
“Kati ya nafasi ambazo zinanipa ugumu wa kupanga
namba kwenye kikosi changu, basi ni safu ya kiungo yenye wachezaji nane ambao
wote wana uwezo wa kucheza soka safi.
“Kiukweli kabisa nakabiriwa na changamoto kubwa
ya kuwapanga viungo hao, lakini kila mmoja nitampanga kutokana na aina ya mechi
nitakayoicheza, nikiamini nikimtumia ataonyesha kiwango kikubwa.
“Ukiwa na idadi kubwa ya wachezaji na wote wenye
uwezo mkubwa, ushindani unaongezeka katika timu kutokana na kila mmoja
kuonyesha uwezo mkubwa ili apate nafasi ya kucheza,” alisema Kerr.
0 COMMENTS:
Post a Comment