Pamoja na
kuonekana inayumba, Prisons imeibuka na kutwanga Mbeya City kwa bao 1-0.
Katika mechi ya
Ligi Kuu Bara leo, Prisons imeibuka na ushindi huo baada ya kupata bao la
kipindi cha kwanza.
Pamoja na
juhudi za Mbeya City katika kipindi cha pili, bado mambo hayakuwa mazuri.
SHINYANGA:
Mjini
Shinyanga, Stand United nayo baada ya kupoteza mechi mbili iliibuka na
kuitwanga African Sports kwa mabao 2-0.
TANGA:
Baada ya kipigo
kutoka kwa Simba cha mabao 2-0 ikiwa nyumbani, Mgambo nayo imeamka na kuichapa
Majimaji kwa bao 1-0.
Majimaji ambayo
ilikuwa haijapoteza hata mechi moja baada ya kucheza mbili na kushinda ikiwa
nyumbani, imeonja utamu wa kipigo baada ya kutandikwa ikiwa ndiyo mechi yake ya
kwanza ugenini, safari hii ikiwa Mkwakwani.
0 COMMENTS:
Post a Comment