Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga amesema uongozi wao
sasa unataka kufanya vitendo zaidi ya maneno.
Sanga amesema anaamini Yanga ina nafasi ya kufanya vizuri katika
mechi yake ijayo dhidi yawatani wao Simba lakini sasa ni vitendo zaidi.
“Kama ukisema maandalizi, naweza kusema tuko vizuri kabisa.
Mwalimu na benchi la ufundi wamepewa kila walichohitaji.
“Kikubwa kwetu sasa ni mapambano na kufanya vitu kwa vitendo,”
alisema.
Tayari Yanga imetia nanga kwa kuanza kambi yake kwenye visiwa vya
Pemba kujiandaa na mechi hiyo dhidi ya Simba.
Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana, Yanga ililala kwa bao
1-0.
Yanga imekuwa ikihaha kurudisha heshima yake ya kuifunga Simba
ambayo sasa inaonekana haina hofu hata kidogo kila inaposikia inakutana na
Yanga.
Kwa mara ya kwanza msimu huu, timu hizo kongwe nchini zinakutana Jumamosi huku kila moja ikiwa imeshinda mechi tatu za mwanzo za Ligi Kuu Bara.







0 COMMENTS:
Post a Comment