November 8, 2015


Kocha Mkuu wa Simba, Dylan Kerr amesema lazima Simba iongeze mshambuliaji ambaye atakuwa ni tishio Tanzania.


Kerr raia wa England amesema kuwa na mshambuliaji tishio ni sehemu ya uimara au uhakika wa kikosi kufanya vema.

Akizungumza na SALEHJEMBE, Kerr amesema kutaka mshambuliaji mkali zaidi haina maana Simba haina washambuliaji wazuri.

“Lazima uwe na kikosi kipana. Kuwa na kikosi kipana maana yake ushambuliaji, beki, kiungo kote kunakuwa na chaguo kubwa.

“Najua katika kipindi cha dirisha dogo nitashirikiana na uongozi kuhakikisha tunatatua mapungufu kadhaa.

“Hili si suala la Kerr au uongozi pekee. Hili ni suala la kila upande,” alisema Kerr.


Simba bado haijawa na mwendo mzuri katika Ligi Kuu Bara ingawa hauwezi kusema ni mwendo mbaya sana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic