Nderemo na vifijo zimeibuka katika UWanja wa
Awassa mjini Awassa baada ya beki Salim Mbonde wa Taifa Stars kujifunga bao
katika dakika ya 90.
Bao hilo limeifanya Ethiopia kupata pointi moja
baada ya matokeo ya bao 1-1 leo.
Sasa Ethiopia imefikisha pointi 4 na inasonga
hadi hatua ya robo fainali.
Mapema Stars ilipata bao lilifungwa na Simon
Msuva baada ya krosi ya Mohammed Hussein kutua kichwani mwa John Bocco kabla ya
kumfikia Msuva aliyemalizia kwa ulaiiini kabisa.
0 COMMENTS:
Post a Comment