Nahodha wa Simba, Mussa Hassan Mgosi amesema kikosi chao bado kina
nafasi ya kubadili mambo na kufanya vizuri na itawashangaza wengi.
Mgosi amesema licha ya kuwa na wachezaji wengi chipukizi, lakini
Simba ina nafasi ya kufanya vizuri Ligi Kuu Bara itakapoanza Desemba 12.
“Unajua watu wengi hawajui kama Simba ina kikosi kizuri, imani
yangu ni tofauti na wengi sana.
“Kikubwa watuamini na mashabiki na wanachama waungane nasi
tupambane,” alisema.
Simba ilianza mazoezi ufukweni huku Kocha Dylan Kerr akiwakimbiza wachezaji kwelikweli.
Lakini sasa tayari imeingia katika programu ya kuutumia mpira
zaidi.
Baada ya mechi 9, Simba iko katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa
Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 21.
0 COMMENTS:
Post a Comment