November 14, 2015

BENTALEB (KUSHOTO) AKIICHEZEA SPURS AKIMILIKI MPIRA MBELE YA ALEX SONG WA WEST HAM UNITED NA CAMEROON.

Kiungo wa Tottenham Hotspur na Algeria, Nabil Bentaleb amesema licha ya kutoijua vyema Taifa Stars na soka la Tanzania, ana uhakika timu yake itapata ushindi katika mchezo wa leo wa kufuzu Kombe la Dunia 2018.


Bentaleb mzaliwa wa Lille, Ufaransa, alisema ana matumaini makubwa ya kuibuka na ushindi mzuri katika mchezo huo utakaochezwa kuanzia saa 10:00 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kutokana na uzoefu walionao.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Bentaleb ambaye alikuwemo katika kikosi cha Spurs kilichotoka sare ya bao 1-1 na Arsenal, wikiendi iliyopita kwenye Ligi Kuu England, alisema: “Ushindi wetu hautokuwa rahisi kwani wengi wetu hatuijui Tanzania vizuri.



“Mimi ndiyo mara yangu ya kwanza kuja Tanzania na sijui lolote kuhusu wachezaji wala soka la hapa, lakini lengo letu kuu ni kupata ushindi na hicho ndicho kilicho kichwani mwangu.

“Tunajua wenyeji wamejipanga ili wasifungwe nyumbani lakini tambua kuwa hii ni mechi ya kufuzu Kombe la Dunia na kila mtu anataka kuandika historia ya kucheza michuano hiyo mikubwa, hivyo kazi itakuwepo.”



Nyota huyo ambaye anaichezea Spurs tangu mwaka 2013, ameichezea Algeria mechi 17 na kufunga mabao matatu tangu alipoitwa kikosini kwa mara ya kwanza mwaka 2014.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic