November 5, 2015

KOCHA CHARLES BONIFACE MKWASA AKIFUATILIA KWA UMAKINI MAZOEZI YA KIKOSI CHAKE
Taifa Stars inashuka dimbani Jumapili kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya University of Pretoria maarufu kama Tucks FC.


Tucks inashiriki Ligi Kuu ya Afrika Kusini na mechi hiyo itakuwa ni sehemu ya maandalizi ya Stars inayotarajia kuivaa Algeria Novemba 14, mwaka huu jijini Dar es salaam.
Kocha Mkuu wa Stars, Charles Mkwasa amesema hiyo ni sehemu ya kuanza kujipanga na kuangalia aina ya uchezaji.

“Umeona tokea tumeanza kambi mazoezi ni makali sana, taratibu tunaanza kupunguza huku tukipata mechi hizo za kirafiki,” alisema Mkwasa akizungumza na SALEHJEMBE jijini hapa.
Jumatatu iliyopita ndiyo Stars imetua Johannesburg kuanza kambini hiyo iliyo katika hoteli ya kisasa yenye utulivu na ulinzi mkali ya Holiday Inn Express.

Hoteli hiyo ipo katika eneo la Woodmead nje kidogo ya jiji la Johannesburg na kuna utulivu mkubwa.


Imekuwa ikijifua katika viwanja vya St. Peters College pamoja na kile cha Edenvale katika kitongoji cha Edenvale pia kipo nje kidogo ya jiji hili kubwa nchini Afrika Kusini.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic