December 10, 2015


Mshambuliaji mpya aliyetua nchini kujiunga na Yanga, Issoufou Boubacar Garba 'Diego' atalazimika kusubiri hadi Kocha Mkuu, Hans van der Pluijm ajiridhishe.


Pluijm ameamua kumchukua Diego katika kikosi cha Yanga kinachokwenda Tanga leo kwa ajili ya mechi mbili za Ligi Kuu Bara.

Ikiwa Tanga, Yanga itacheza dhidi ya Mgambo Shooting Jumamosi kabla ya kuivaa African Sports.

Hivyo, Pluijm atatumia muda wa mazoezi ya timu kuangalia uwezo wa mshambuliaji huyo kutoka Afrika ya Kati.

Yanga imeamua kumuacha Coutinho raia wa Brazil ili kumpata mshambuliaji mbadala na Diego ni kati ya wanaovizia nafasi hiyo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic