December 13, 2015



Yule mshambuliaji Javier Harnandez alionekana hafai kwa kocha Louis van Gaal, ameoyesha yuko sawa kwa kutupia mabao matatu au hat trick wakati timu yake ya Bayer Leverkusen ikishinda 5-0 dhidi ya Borussia Monchegladbach ya mechi ya Bundesliga.

Borussia Monchegladbach ndiyo wale walioifunga Bayern Munich baada ya kuitwanga kwa mabao 3-1, lakini sasa nao wamepata mbabe.

Wakati Harnandez maarufu kama Chicharito akipiga bao hizo tatu, Manchester United ilikuwa ‘inachezea’ kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa kibonde Bournemouth katika Premier League.

Bayer Leverkusen:
Leno, Hilbert (Donati 45), Tah, Toprak, Nascimento Borges, Bellarabi, Kramer, Kampl (Frey 87), 10 Calhanoglu, Hernandez (Mehmedi 79), Kiessling.
Subs not used: Ramalho, Papadopoulos, Kresic, Yurchenko.
Goals: Kiessling 30 and 66, Hernandez 63, 75, 76


Borussia M'gladbach:
 Sommer, Jantschke, (Elvedi 45), Christensen, Nordtveit, Korb, Dahoud (Schulz 81), Xhaka, Wendt, Traore (Raffael 45), Stindl, Drmic.
Subs not used: Brouwers, Hazard, Sippel, Hrgota.
Booked: Jantschke, Korb
Ref: Tobias Stieler
Att: 30,210









0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic