January 7, 2016



Nahodha wa Azam FC amewaomba radhi mashabiki wa kikosi hicho kutokana na kuboronga katika michuano ya Mapinduzi.

Azam FC imetolwa hatua ya makundi baada ya kushika mkia katika Kundi B kwa kutoka sare mbili na kupoteza mchezo mmoja hivyo kubaki na pointi mbili tu. Haya ndiyo maneno ya Bocco aliyoyatupia kwenye mtandao wa kijamii.

"Napenda kuchukua nafasi hii kuwaomba radhi mashabiki wote wa Azam Fc kwa performance mbaya tulioonyesha kwenye mashindano ya Mapinduzi na mechi mbili za Ligi kabla ya kuja huku, matokeo ni sehemu ya mchezo inakubalika, lakin kitu kinacho angaliwa ni unapataje matokeo yawe mazuri au mabaya.

"Tumepata matokeo mabaya kutoka kwenye performance mbaya zaidi kuwahi kuiona katika timu yetu tangu nilipoanza kucheza hadi sasa hivi, hivo tunawaomba radhi mashabiki wetu wote na kuwaaidi tutajituma na kupigania club yetu kwa moyo wetu wote."

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic