January 7, 2016


Balozi wa Tanzania nchini Nigeria, Daniel Ole Njoolay amesema ana imani kubwa Mtanzania, Mbwana Samatta atashinda tuzo ya Mwasoka Bora Afrika.

Samatta anawania tuzo ya mwanasoka bora Afrika kwa wale wanaocheza soka ndani ya bara hilo. 
Njoolay amezungumza na Radio One na kuiambia Samatta amewasili  salama na wana matumaini makubwa atafanya vizuri.


OLE NJOOLAY

"Amewasili hapa jana saa saba, tumempokea, anaonyesha ni mwenye furaha na kwa kweli tuna matumaini atafanya vizuri," alisema Njoolay.

Samatta ameingia fainali na kipa mkongwe wa TP Mazembe, Muteba Kadiaba na mshambuliaji wa Etoile Du Sahel, Bouned Baghdad raia wa Algeria.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic