Simba walijiamini wangeitandika Yanga, lakini mambo yakageuka na wao kupoteza kwa kufungwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, jana.
Upande wa jukwaa kubwa yaani VIP, wengi walikuwa viongozi wa Simba na wadau wengine wa karibu.
Kwa muda wote wa mchezo walionekana wakiwa wamelowa kabisa tena ile mbaya. Walikuwa watulivu kama vile wamemwagiwa maji.
Hofu kwao ilianza kuonekana baada ya dakika ya 25 pale beki Abdi Banda alipolambwa kadi ya nyekundu.







0 COMMENTS:
Post a Comment