April 13, 2016


MPIRA UMEKWISHAAAA -Yanga inapata kona baada ya krosi ya Niyonzima kuokolewa, inachongwa lakini haina madhara
-Juma anapiga shuti kali kabisa kupitia mpira wa faulo, lakini mpira unatoka pembeni ya lango la MWadui

DAKIKA 3+ ZA NYONGEZA
Dk 87 hadi 80, Yanga wanaonekana kumiliki mpira zaidi huku MWadui wakionekana kupoteza uchezaji wao kama vile wamekubali
GOOOOOOOOO Dk 86, Niyonzima anaifungia Yanga bao la pili kwa shuti kali kabisa baada ya kuukuta mpira ukiambaaDk 84 Kado kwa mara nyingine anaokoa mpira wa kichwa wa Busungu na kuuchukua kwa mbwembwe kabisa
Dk 83, Sabati anageuka vizuri mbele ya Cannavaro anapiga shuti kuuuubwaaaa
Dk 81, mabeki na viungo wa Mwadui wanafanya kosa kwa kuuangalia tu mpira, Busungu anapiga shuti kali lakini linatoka sentimeta chache pembeni ya lango la YangaDk 79, shuti la Msuva lakini Kado anaonyesha umahiri mkubwa kabisa tena
SUB 78, Yanga wanamtoa Tambwe nafasi yake anachukua Malimi Busungu
Dk 78Dk 75, Nizar anapokea pasi nzuri ya Malika Ndeule, anageuka na kupiga shuti kali lakini linakuwa hafifu

Dk 71 hadi 72, pamoja na mchezaji wao mmoja kutolewa lakini Mwadui FC wanaonekana kuwa watilivu na kucheza mpira vizuri kabisa
KADI Dk 70, Iddi Mobi anacheza rafu ya kijinga kabisa, anamuangusha Ngoma na mwamuzi anampa kadi ya pili ya njano na kuwa nyekundu, anakwenda nje

Dk 67, krosi nzuri ya Msuva, Kado anajichanganya na Malika lakini anaruka na kuudaka tena mpira huo
Dk 64, Tambwe anaruka na kupiga kichwa safi lakini mpira unapita juu kidogo ya lango la Mtibwa Sugar
Dk 61, Kado anaonyesha umahiri mwingine kwa kudaka shuti kali la Niyonzima akipokea pasi ya Ngoma

DK 58 Msuva anapiga shuti safi kabisa, lakini Kado anaonyesha umahiri na kuokoa, mpira unagonga mwamba na kurudi uwanjani
SUB Dk 57 Mwadui wanamtoa Hassan Kabunda na nafasi yake inachukuliwa na mkongwe Nizar Khalfan
Dk 51 hadi 54, Mwadui FC wanaonekana wako vizuri zaidi katika sehemu ya kiungo
Dk 50, Yanga wanapoteza nafasi ya kufunga baada ya Ngoma kuruka na kupiga kichwa lakini mpira unatoka nje

SUB Dk 46, Yanga wanamtoa Pato Ngonyani nafasi yake anachukua Vicent Bossou, Gofrey Mwashiuya anachukua nafasi ya Issouf Aboubacar

MAPUMZIKO
Kipindi cha kwanza kimemalizika kwa timu hizo kupata bao moja kila moja.


yanga ilianza kupata bao katika dakika ya 3 kupitia Simon Msuva na Mwadui FC wakasawazisha katika dakika ya 13 kupitia Kelvin Sabato.

2 COMMENTS:

  1. Mbona balaaa hili vyote vina cheza

    ReplyDelete
  2. Yanga kila mchezaji ni wa kutegemewa na akipata nafasi anafunga,sio sisi Simba kuwa na ndoto na kiiza tu hata akifanya utovu wa nidhamu hapewi adhabu mnamlewesha sifa,kachelewa wiki nzima hakuna maelezo badala yake kaonekana anacheza,eti na gari kazawadiwa,niliwapenda yanga walivyokuwa na msimamo kwa Niyonzima wakati amechelewa kurudi toka kwao,na inapendeza mchezaji unapata mshara mkubwa lazima uheshimu.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic