June 18, 2016


Mabosi wa Simba kiroho safi walikubaliana kumsajili beki wa kati wa Prisons, Nurdin Chona, lakini beki huyo akataka asajiliwe kwa dau la Sh milioni 40, Simba ikanywea, ikatulia.

Kwa kuwa Simba wana shida, wakambembeleza Chona awashushie bei, lakini beki huyo akaendelea kubaki palepale kwamba anataka Sh milioni 40. Simba ikaona isiwe shida ikaachana naye.

Hesabu za Simba zilikuwa ni kumsajili Chona ili kuimarisha safu yake ya beki ya kati ili aweze kushirikiana na Novatus Lufunga na Juuko Murshid. 

Baada ya kuona mambo yanashindikana, Simba ikazungumza na beki wa Mwadui FC, Emmanuel Semwanza ambaye alikubali kusaini kwa Sh milioni 20 tu kwa mkataba wa miaka miwili. Mambo yakaishia hapo.

Hebu sikia kilichotokea baada ya Semwanza kusajiliwa, mmoja wa mabosi wa Simba alisema: “Aliposikia tumemsajili Semwanza, eti Chona akatuomba tumsajili hata kwa Sh milioni 20.

“Tukamjibu palepale kwamba, basi haitawezekana maana tumeshampata mbadala wake na mambo yakaishia hapo, kilichomponza ni tamaa tu,” alisema bosi huyo.

Licha ya Chona, Simba bado inahusishwa na taarifa za kumnyakua Salum Kimenya wa Prisons.


Alipotafutwa Chona alisema: “Ni kweli Simba tuliongea lakini hatukifikia mwisho, tulipishana kwenye kipengele cha maslahi lakini pia ishu ya mkataba wangu na Prisons ilichangia. Nina mkataba mrefu wa miaka minne, hivyo kwa kiasi kikubwa nao ulichangia tusifikie mwisho wa mazungumzo yetu.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic