September 27, 2016



Kocha Joseph Omog amekomalia suala la upotezaji wa nafasi ambalo limekuwa kubwa katika kikosi chake cha Simba.

Simba imeweka kambi mjini Morogoro, ikifanya maandalizi dhidi ya mechi ya watani wake Yanga, Oktoba Mosi.

Katika mazoezi yake, Omog amekuwa akiwasisitiza wachezaji wake kufunga ikiwezekana kwa asilimia 90 katika nafasi wanazozipata.

Kwani kila wanapofika kwenye eneo la lango, amekuwa akisimamisha mpira na kuwasiistiza namna ya kuzitumia nafasi.


Simba imekuwa ikipoteza mechi zake nyingi za kufunga kila inapokuwa inashambulia katika mechi mbalimbali za ligi inazocheza.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic