September 18, 2016

Baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Watford kwa mabao 3-1, Kocha wa Manchester United amedai kuwa makosa binafsi ya wachezaji wake yamesababisha hali hiyo pamoja na kumtupia lawama mwamuzi katika bao la kwanza.





 Pamoja na kusema hivyo, amesisitiza kuwa vijana wake wote wanatakiwa kufika mazoezini kesho asubuhi na kuendelea na ratiba ya mazoezi huku muda wa kupumzika siku moja baada ya mechi kama ilivyo kawaida ukiwa haupo.


 

"Kesho tutakuwa na mazoezi saa 4.30 asubuhi, tunatakiwa kuwa pale ili kufanya kazi kuonyesha hatupo kwenye hali nzuri.

"Tunahitaji mawazo chanya ya kutuongoza ili mechi ijayo wakiingia uwanjani wajue tunaenda kufanya kazi gani."


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic