January 8, 2017


Baada ya Yanga kupoteza kwa mabao 4-0 dhidi ya Azam FC, Simba imesema itaendelea kuchukua tahadhari kubwa kwa kila mechi yake ya Kombe la Mapinduzi.

Simba imeshinda mechi zake zote za Mapinduzi lakini haikuwa ikishinda kwa idadi kubwa ya mabao kama ilivyo kwa Yanga.

Simba inashuka dimbani Amaan mjini Zanzibar kuivaa Jang’ombe Boys katika michuano hiyo.

Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja amesema wako tayari na wanachotaka ni kufanya vizuri.

“Kila mechi ni mechi nyingine, lazima kuwa makini kwa lengo la kufanya vizuri,” alisema.

Simba inaongoza Kundi A ikiwa na pointi saba baada ya kushinda mbili na sare moja.


Iwapo itashinda leo, uhakika asilimia mia kuivaa Yanga katika nusu fainali utakuwa umepatikana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic