January 18, 2017



Baada ya mwanariadha Mtanzania, Alphonce Simbu kufanikiwa kuibuka mshindi wa mbio za Mumbai Marathon, wikiendi iliyopita, Chama cha Riadha Tanzania (RT), sasa kimempa jukumu la kwenda London kuchukua medali nyingine.

Simbu ambaye kwenye mbio hizo alifanikiwa kushika nafasi ya kwanza na kuondoka na medali pamoja na kitita cha dola 67,000 ambazo ni sawa na Sh milioni 147 za Kitanzania, Agosti mwaka huu anatarajiwa kushiriki mbio za World Athletic Championship zitakazofanyika London, England.


Juzi Jumatatu, mwanariadha huyo alitua nchini kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na siku yoyote anatarajia kutua jijini Dar ambapo ataandaliwa tafrija ya kupongezwa na wadhamini wake, Kampuni ya DStv.

Katibu Mkuu wa RT, Wilhelm Gidabuday, ameliambia Championi Jumatano kuwa: “Fedha alizopata zimegawanyika sehemu tatu na kufikia hizo dola 67,000, zawadi za mshindi wa kwanza ni dola 42,000, lakini kutokana na kufanya kwake vizuri kwenye Olimpiki alipata mwaliko maalum ambao ulikuwa na kipengele kwamba akishinda au akishindwa lazima apewe dola 15,000 na wastani mzuri wa kukimbia akapata bonasi ya dola 10,000.


“Kilichobaki sasa tunataka aende London kwenye mashindano ya World Athletic Championship na kurudi na medali, tukipata medali huko ni heshima kubwa kwani haya ni ya pili kwa ukubwa ukiondoa Olimpiki.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic