Prisons imeendeleza ubabe wake kwa Mbeya City baada ya kuitwanga kwa bao 1-0 katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, leo.
Prisons ilionyesha soka safi tokea mwanzo, lakini Mbeya City wakafanya mashambulizi mengi ingawa kipa wa Prisons akawa kipingamizi kikubwa kwao kupata bao.
Wakati Prisons wakiitwanga Mbeya City, upande mwingine mechi iliyokuwa ipigwe Nangwanda Sijaona mjini Mtwara kati ya wenyeji Ndanda FC na Majimaji
Majimaji ambao ni majirani wa Ndanda, walichelewa kufika mjini Mtwara na sasa mechi hiyo itapigwa kesho.
0 COMMENTS:
Post a Comment