February 9, 2017


BAADHI YA WAHUBIRI KUTOKA KATIKA KANISA LA GWAJIMA

Taarifa zinaeleza Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji na Mchungaji Josephat Gwajima wameondolewa katika kitu Kikuu cha Polisi cha Dar es Salaam.

Mmoja wa mashuhuda amesema Manji na Gwajima wanaweza wakawa wamepelekwa kupimwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali au Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

“Ni kweli hii saa kumi na nusu au zaidi, wameondolewa hapa kituoni. Wawili wamepanda gari aina ya Land Cruiser wakiongozana na askari Polisi kadhaa.


“Gari limeondoka na kuekelea maeneo ya Posta ya zamani. Huu uelekeo huenda kwenye ofisini za mkemia mkuu. Lakini hakuna mwenye taarifa rasmi,” kilieleza chanzo.


Manji na Gwajima walifika kwa ajili ya kuhojiwa kuhusiana na suala la madawa ya kulevya baada ya kutuhumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic