February 14, 2017




Kocha Mkuu wa timu ya Soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Mayanga amekabidhi programu ya miezi sita kwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Salum Madadi akianzia mechi ya kirafiki za kimataifa kabla ya mechi za ushindani.


Mechi hizo ni kwa za wiki kwa mujibu wa Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na kalenda ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) ambako kwa kuanzia tu, ataanza maandalizi ya mechi za wiki ya FIFA ambazo zitachezwa kati ya Machi 21 na 29, mwaka huu.


TFF bado inaratibu michezo dhidi ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro kwa maana ya wapinzani wao hapo baadaye.


Mwezi Aprili, kati ya tarehe 20 hadi 22, 2017 kutakuwa na mechi za kufuzu kwa michuano ya kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaokipiga Ligi ya Ndani (CHAN) ambako Taifa Stars itacheza na Rwanda katika hatua za awali. Fainali za CHAN zitafanyika Kenya mwakani.


Kwa mujibu wa ratiba, Juni 6 hadi 13, mwaka huu kutakuwa na mechi za kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) dhidi ya Lesotho katika mchezo utakaofanyika hapa Tanzania.



Kwenye AFCON Tanzania iko kundi “L” ambalo wapinzani wake wako Lesotho watakaoanza kucheza nao hapa nyumbani kabla ya huko mbele kucheza na Uganda na Carpe Verde. Fainali za AFCON zinatarajiwa kufanyika Cameroon, mwaka 2019.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic