March 1, 2017




Na Dr Haroun Haroun

Yanga  ina  daktari wa  timu  anaitwa  Dr Edward bavu nafikiria  ana  taaluma  ya  kutibia  wachezaj  vizuri, lakini  wakati  mwingine kwa sisi madaktari ikitokea ukishindwa kumtibu mgonjwa unaweza kuomba  daktari  mwenzio akusaidie.

Nilipigiwa  simu  na  Mjumbe  mmoja  wa  yanga ili  nimsaidie  kumtibu Donald Ngoma baada ya kutoka Zanzibar , Nilifanya  hivyo  nafikiria  hii inatokana  na weledi wangu mzuri  wa  uelewa  katika  taaluma  ya  matibabu  ya  michezo, nilimpokea nikamfanyia vipimo pamoja na matibabu (angalia picha na maelezo ya tiba hapo chini).

Nimewasaidia  wachezaji  wa  yanga  waliokuwa  na  shida  mbalimbali za kimatibabu hasa  yale  yaliyokuwa  sugu  katika  michezo (Hissan) wewe ni shahidi, nina  reference  ya Mwashiuya, Juma  Abdul  na Canavaro pamoja na  wachezaj  wengine  mbalimbali  sijawahi  lalamikiwa  hata  siku  moja.

Nilimtibu  Kwa  muda  wa  wiki  mbili  kwa  jeraha la goti  na  kupona  kabisa ,nakumbuka  tarehe  3 Februari,  Yanga  walicheza dhidi ya Stand United  nikiwa nyumbani naangalia mchezo huo ambao Ngoma aliumia na kushindwa kuendelea na mchezo, baadaye nikamwandikia sms kwa  Whatsap  kujiridhisha  kama  bado  jereha  linamsumbua,? akasema, hapana  anachoumwa  Sasa  ni  groin  ikiwa  na maana  kiuno  au  wengine  hupenda  kusema  nyonga na alinijibu Kwa  whatsap  SMS (screen shot nimekutumia), nikamuahidi  kumsaidia  tena  kwa  tatizo  hilo,baada ya matibabu akasema  anajisikia  amepona  na  hata  majibu  ya  vipimo  hayakuonyesha tatizo (picha za vipimo na matibabu hizo nimetuma). 

Kitaalamu  Kuna  aina  nne  ya  matibabu  katika  mpira, kuna  sports medicine doctor, physiotherapy, sport nutrition advisor na  chiropractor  ambayo  tunaita  matibabu  mkandamizo  utaalam  huu  nchi  yetu  Hakuna, Ngoma  aliwaongopea  viongozi  wa  Yanga SC  kwa  kuja  na  report  ya  kutengenezwa  kutoka  London  Health  ambayo  imeandikwa  na  physiotherapy  na  siyo  daktari  wa  Michezo.

Fomu  ya  FIFA  ina  sehemu ya daktari  wa  timu na  daktari wa viungo, daktari  wa  viungo  hawez  kuandika  report  Ya  Mchezaji  itakuwa  mara  ya  kwanza  Tanzania.

Ukitazama  report  ya  London  Health  haiko  kwenye maandishi  ya  kidaktari  kabisa inaonekana ilikuwa  mahitaji  ya  Mgonjwa, report  ya  Medical  ina  sehemu  tatu, historia  ya  mgonjwa  ,vipimo  na  ugonjwa  ulioonekana  na  matibabu  yaliyofanyika ambapo daktari  wa  mazoezi  atachukua  report  kutoka  Kwa  daktari.

Niliwaambia ukweli viongozi wa Yanga SC na wewe ukiwemo uliponiuliza (Februari 18) juu ya tatizo lake, nikawajibu kuwa amepona na hana tatizo lolote kiafya hicho ndicho kilichomkasirisha Ngoma na kuamua kunichafua, ukweli ndio umenifanya mimi kuchafuliwa.

Sio kitu  kizuri  kuonyesha  report  ya  Mgonjwa  lakini  hamna  namna, nataka uma wa wana Yanga na wapenzi wa mpira waujue ukweli kuhusu Ngoma, Yanga SC wamekuwa wanaleta  wagonjwa  kwangu  wakati  wana  daktari  wa  timu hii  inaonyesha  ubora  wangu  wa  kazi na imani waliyonayo kwangu, sio jambo jema kwangu kulikalia kimya jambo ambalo linahatarisha mustakabali wa taaluma yangu.


Niwaombe radhi wote niliowakwaza kwa namna moja ama nyingine, nawaomba mliokuwa na imani muendelee kuniamini na sitowaangusha, imani yenu kwangu isipotee kwa jambo hili.

1 COMMENTS:

  1. Mimi naona huyu mchezaji hatufai yanga tunaonata mafanikio Leo unakuwa na mtu ambae hana uchungu na timu.Ngoma hajitumi uwanjani ukilinganisha na alivokuja yanga.Tumfungulie mlango wa kutokea,Tuna wachezaji wazawa wenye mchango mkubwa kwenye timu kama Msuva kuliko hata huyo ngoma.aende zake

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic