Method Mwanjale anatarajia kuanza mazoezi katika kikosi cha Simba, kesho.
Beki huyo wa kati wa Simba, amerejea jana akitoka kwa Zimbabwe ambako alikwenda baada ya kuwa majeruhi.
Mwanjale raia wa Zimbabwe amekuwa akisumbuliwa na maumivu yaliyomfanya kukaa nje kwa zaidi ya wiki mbili.
“Sasa yuko vizuri kabisa, siku zake za kupumzika zimeisha na ziada pia. Hivyo kesho anaweza kuanza mazoezi,” zilieleza habari kutoka ndani ya Simba.
0 COMMENTS:
Post a Comment