April 17, 2017





Wachezaji wa Yanga wanatarajia kuondoka leo usiku nchini Algeria kurejea nyumbani.

Sasa wanatarajia kuondoka na ndege ya Emirates badala ya Turkish Airways na imeelezwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limelazimika kutoa mkopo kwa klabu hiyo ili kuwakomboa.

Wachezaji saba na Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa walichelewa ndege jijini Algeria na kulazimika kusubiri hadi Jumanne kesho ndiyo waondoke na kutua nchini kesho.

Mkwasa alisema wataomba msaada kwa MC Alger waliokwenda kucheza nao na kufungwa mabao 4-0 kwa kuwa hawakuwa na fedha za kutosha.


Lakini msaada huo wa TFF utawafanya warejee haraka nyumbani na si Jumatano tena kama ambavyo ilikuwa ikitarajiwa.

1 COMMENTS:

  1. Kushangaa shangaa kwingi mpaka wanasahau kurudi nyumban

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic