May 22, 2017



Baada ya kuukosa ubingwa wa ligi, benchi la ufundi la Simba chini ya kocha wake, Joseph Omog, raia wa Cameroon, limeweka wazi kuwa litajipoza machungu yake kwa kuifunga Mbao kwenye mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho (FA) ili kujipatia nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani.

Omog na Simba yake walishuhudia wapinzani wao wakuu Yanga wakichukua ubingwa wa ligi kwa msimu huu licha ya wote kuwa na pointi 68, lakini wapinzani wao hao wamewapita kwa idadi ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Mcameroon huyo ameliambia gazeti hili kuwa, hawajakata tamaa juu ya kikosi chao kutwaa ubingwa katika msimu huu, baada ya kuikosa ligi kwani sasa ameelekeza ujuzi wake kuhakikisha anaisaidia timu hiyo kuchukua FA.

“Kila mmoja ameona jinsi ambavyo tulipambana tangu mwanzo wa ligi mpaka mwisho wake ambapo tumekosa ubingwa kwa tofauti ya mabao pekee, lakini nia yetu ilikuwa ni kuutwaa ubingwa ili tujikatie nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa.

“Lakini hiyo siyo kitu kwa sababu licha ya kukosa kwa njia hiyo ya kuchukua ligi, kwa sasa tuna mechi ya fainali mkononi ambayo hiyo tunataka kuitumia kwa ajili ya kupoza machungu yetu ya kukosa ubingwa lakini pia kujipatia nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa ambapo mara ya mwisho ilikuwa miaka mitano nyuma,” alisema kocha huyo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic