June 14, 2017


Baada ya kufutwa utaratibu wa mawakala ‘agents’ wa wachezaji wa kulipwa, Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), lilitangaza utaratibu mpya wa kukasimu majukumu hayo kwenye ngazi ya mashirikisho kwa kila taifa.

Hivyo kwa mwaka 2016/2017, hakuna usajili wala uhamisho uliofanywa na watu wa kati yaani intermediaries wanaotambulika na TFF.

TFF - Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, linakwenda sambamba na utaratibu huo wa mabadiliko na kwa sasa linakamilisha mipango ya kusajili watu wa kati wa usajili watakaofahamika kama intermediaries.


Usahili wa kati utatangazwa baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji kitakachojadili kanuni za watu wa kati hapo baadaye.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic