June 14, 2017





Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), linawaalika wanafamilia wote wenye nia ya kuwania uongozi katika shirikisho kujitokeza kuchukua fomu kuanzia Juni 16, mwaka huu.

Tarehe hiyo ni ileile iliyotangazwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Wakili Revocatus Kuuli alipozungumza na wanahabari Jumatatu wiki alipotangaza ratiba nzima ya Uchaguzi Mkuu wa TFF uliopangwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu.

Kwa kuwa tovuti ya TFF: www.tff.or.tz kwa sasa ipo kwenye marekebisho, zoezi la kuchukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi TFF zitatolewa kwenye ofisi za TFF zilizopo Ilala, Dar es Salaam kuanzia asubuhi ya Juni 16, 2017 hadi saa 10 jioni siku ya Juni 20, mwaka huu.

Fedha za kulipia fomu hizo zitalipiwa Benki ya CRDB kupitia namba ya akaunti 01J1019956700 ambako mgombea atawajibika kuwasilisha stakabadhi ya malipo kutoka benki na kupewa fomu ya nafasi husika.

Gharama za kuchukulia fomu ni.
1.   Rais TSh 500,000/=
2.   Makamu wa Rais Tsh 300,000/=

3.   Wajumbe wa kamati ya utendaji Tsh 200,000/=

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic