June 24, 2017


MEYA WA UBUNGO, BONIFACE JACOB (MWENYE KIBARAGASHIA), AKIWA NA WANYAMA.

Meya wa Manispaa ya Ubongo Boniface Jacob, amemtunuku mtaa, Kiungo wa Tottenham ya England Victor Wanyama raia wa Kenya.

Jacob ambaye ni Meya akitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameonekana kufurahishwa na mchezaji huyo kufika katika eneo lake na kuunga mkono michezo.



Hivyo kwa kufurahishwa na namna alichofanya kiungo huyo Mkenya ambaye ni nahodha wa Harambee Stars ameamua kumzawadia Barabara.

Wanyama amepewa jina la mtaa uliyokuwa katika mtaa uliokuwa ukifahamika kwa jina la  Viwandani.

Kabla, Wanyama alihudhuria mashindano ya Ndondo Cup yanayoendelea katika Uwanja wa Kinesi Ubungo Shekilango jijini Dar es Salaam jioni hii. 



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic