July 23, 2017



Mshambuliaji mpya wa Yanga, Ibrahim Ajibu amezua mjadala kwenye mtandao wa kijamii baada ya kutuma ujumbe akimshukuru Mungu na kusema anajiamini.

Baada ya hapo mashabiki wameanza kutuma maoni yao kila mmoja akisema yake lakini walioonekana ni wa Simba, walikuwa wakimshangaa au kumlaumu kuhama huku wengine wakimuita ni msaliti.

Waliomuita msaliti walisema amehama lakini hataweza kucheza soka katika kiwango bora.

Lakini wale walioonekana ni wa Yanga walimpa moyo na kumtaka acheze bila ya woga kwa kujituma huku wakimkaribisha.

Baadhi yao walifikia kushangazwa na wale waliiwaowahi kumuita anajua sana akiwa Simba lakini kwa kuwa amehama anaonekana hana lolote.

Wakati mwingine, mashabiki hao walianza kubishana au kuzoana wao kwa wao wengine wakionyesha kuwa na jazba wakati wakiwajibu wengine.


Pamoja na rundo la maoni, Ajibu aliendelea kuwa kimya bila kusema lolote.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic