Azam FC wamesema wamepania kupata pointi tatu dhidi ya Mwadui FC mechi itakayochezwa wikiendi ijayo.
Msemaji wa Azam FC, Jaffar Iddi anasema wameishatua mjini Shinyanga kwa maandalizi ya mwisho ya mechi hiyo.
"Tunaichukulia mechi hiyo kwa uzito mkubwa, tunazitaka pointi tatu," alisema.
Kabla ya mechi hiyo, Azam FC ilipoteza pointi mbili za ugenini baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Singida United kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
0 COMMENTS:
Post a Comment