October 10, 2017



Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi katika kikao chake kilichopita ilipitia taarifa na matukio mbalimbali ya Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili msimu wa 2017/2018 zinazoendelea hivi sasa.

Katika taarifa hizo imebainika kuwa timu yako haikuhudhuria katika kikao cha maandalizi (pre match meeting), na pia ilichelewa kufika uwanjani wakati wa mechi namba 3 ya Kundi C dhidi ya Boma FC iliyochezwa Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa Mwakangale uliopo Kyela mkoani Mbeya.

Kitendo hicho ni ukiukaji wa Kanuni ya 14(2a) na Kanuni ya 14(9) za Ligi Daraja la Pili. Kwa vile ni kosa la kwanza kwa timu yako msimu huu, Kamati imeipa klabu yako Onyo Kali kwa kuamini kuwa kosa hilo la kikanuni halitajitokeza tena. Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 14(3) na 14 (48) za Ligi Daraja la Pili.


Unakumbushwa kuwa Ligi Daraja la Pili inaendeshwa kwa kuzingatia Kanuni husika, na ni matarajio yangu kuwa ukiwa mtendaji mkuu wa klabu utakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kanuni hizo zinafuatwa kikamilifu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic