October 10, 2017






Kamati ya Bodi ya Ligi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imemuondoa Mwamuzi Msaidizi Grace Wamara kuchezesha Ligi Kuu ya Vodacom kwa kukosa umakini na kutomsaidia Mwamuzi, hivyo kusababisha akubali bao lenye utata la Stand United dhidi ya Mbeya City.

Wamara alikuwa Mwamuzi Msaidizi Namba Mbili kwenye mechi hiyo namba 31 iliyofanyika Septemba 24 mwaka huu kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga na wenyeji Stand United kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Uamuzi wa kumuondoa Wamara ambaye amerejeshwa katika Kamati ya Waamuzi ya TFF kwa ajili ya hatua nyingine umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 38(5) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Waamuzi.


2 COMMENTS:

  1. Kichwa cha habari na maelezo ni tofauti kabisa, zijui Mavugo katika habari anafiti wapi?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic