December 28, 2017



Ramani ya msiba

Msiba uko nyumbani kwake Mbweni Kijijini, Dar es Salaam, eneo la Mbweni Maputo,siyo mbali na hospitali ya Mbweni Misheni.

Yaani ukiwa unatokea Mwenge unapanda daladala ziendazo Mbweni Kijijini, unashukia kituo cha Mbweni Misheni, kisha hatua chache mbele kuna njia inayokwenda kushoto ituate barabara hiyo kwa kuongozwa na vibao vinavyoelekeza msiba ulipo mpaka utakapofika nyumbani kwa marehemu, ambaye ni maarufu kama Mzee Magazeti.

Njia nyingine ni kupanda mabasi ya Makumbusho-Bunju/Bagamoyo, shukia  kituo cha Mianzini Bunju.
Hapo chukua bodaboda kwa gharama ya kama 3000/= hadi mbele kidogo ya Mbweni Misheni Hospitali. Ukifika hapo kata kushoto na muelekeze huyo bodaboda afuate vibao vya kuelekeza msiba hadi nyumbani kwa marehemu.

Kwa wenye usafiri binfsi; unaweza kufika kwa njia mbili:

1.Ukitoka Mwenge nenda mpaka Petrol Station ya Lake Oil eneo la Bunju. Hapo kuna barabara ya lami kuelekea Mbweni. Ifuate hadi Mbweni Kijijini,utakapoikuta Hospitali ya Misheni Mbweni. Baada ya hapo kata kushoto.Fuata vibao vya msiba vitakufikisha. 

2.Ukitoka Mwenge nenda hadi njia panda Mbweni Jeshini, fuata njia ya daladala, yapite mageti ya Jeshi hadi Mbweni Kijijini.Endelea mbele hadi Mbweni Misheni Hospitali.Sogea mbele kidogo, halafu kata kushoto na anza kufuata maelekezo ya vibao vya msiba ambavyo vitakufikisha.

Usafiri kwa Wanahabari

Kwa mujibu kamati ya maandalizi kutakuwa na mabasi mawili ya UDA yatakayobeba wanahabari watakaokwenda kumuaga mwenzao.

Basi la kwanza litakuwa Idara ya Habari Maelezo,Mtaa wa Samora, kuanzia saa 1:30 asubuhi ambapo litaondoka saa 2:30 kuelekea msibani Mbweni.

Basi la pili litakuwa Mwenge,maeneo ya kituo cha mafuta cha BP, kuanzia saa mbili asubuhi ambapo litaondoka hapo saa 3 kuelekea msibani.

Poleni sana,

Imetolewa na Kamati ya Maandalizi

Desemba 27, 2017.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic