December 8, 2017



Kutokana na beki wake, Juuko Murshid kuonekana ni lulu na kuzivutia timu kadhaa wakiwemo watani wao Yanga, Simba wameanza kujipanga.

Taarifa zinaeleza, Simba imeamua kumtuma mjumbe kwenda Kenya ambako Juuko anaitumikia timu yake ya taifa ya Uganda katika michuano ya Chalenji.


"Lengo ni kuzungumza naye mambo kadhaa na kumueleza msimamo wa Simba. Unajua mengi yanazungumzwa na huenda yakasababisha aelewe tofauti," kilieleza chanzo.

"Siku zinakwenda na Juuko anajua kwamba Simba bado inamhitaji lakini si vibaya kukutana naye na kuzungumza naye."

Yanga ni kati ya timu zilizoonyesha nia ya kuimarisha safu yake ya ulinzi kwa kumnasa Mganda huyo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic