February 2, 2018




KMC imeongeza idadi ya timu zinazotokea Dar es Salaam katika Ligi Kuu Bara baada ya ushindi wake wa bao 1-0 dhidi ya JKT Mlale waliokuwa vinara wa Kundi B la Ligi Daraja la Kwanza.

Ushindi huo unaifanya KMC kupanda Ligi Kuu Bara kwa mara ya kwanza huku shujaa wake akiwa ni kiungo mkongwe Abdulhalim Humud aliyefunga bao hilo pekee.

Huenda furaja kuu itakuwa kwa kocha Fred Felix Minziro maarufu kama Majeshi ambaye aliipandisha Singida United na sasa amejiunga na KMC na kuipandisha pia.

JKT Mlale iliyokuwa nyumbani ilionekana ina nafasi kubwa zaidi ya kupanda kwa kuwa ndiyo ilikuwa kinara ikiwa na pointi 25 sawa na KMC.


Lakini ushindi huo wa KMC umeifanya ifikishe pointi 28 na kupaa kileleni ikifuatiwa na Coastal Union iliyoshinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Mawezi mjini Morogoro. Coastal imemaliza ikiwa na pointi 26 wakati Mlale wanabaki na 25.


KUNDI B
                                P   W   D   L   F   A  GD  Pts
1. KMC                     14   8   4   2   17  13  4    28
2. Coastal Union       14   7   5   2   18   9   9   26
3. JKT Mlale             14   7   4   3   13   7   6   25
4. Polisi Tanzania     14   6   6   2   18   12  6   24
5. Mbeya Kwanza      14   6   4   4   14   10  4   22


6. Mufindi                 14   3   4   7   13   21 -8  13

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic