February 2, 2018




Kikosi cha Wagosi wa Kaya au Coastal Union kimerejea Ligi Kuu Bara baada ya kuandika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mawenzi.

Katika mechi yake hiyo ya pili iliyopigwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, Coastal Union iliiripua Mawenzi kwa mabao hayo mawil, moja likifungwa na kiungo mkongwe Athumani Iddi ‘Chuji’.
Raizin Ally ndiye aliandika bao moja na Chuji aliyewahi kung’ara na Yanga na Simba akapiga msumari mwingine.

Kwa ushindi huo Coastal Union imefikisha pointi 26 na kujihakikishia kurejea Ligi Kuu Bara.

KUNDI B
                                P   W   D   L   F   A  GD  Pts
1. KMC                     14   8   4   2   17  13  4    28
2. Coastal Union       14   7   5   2   18   9   9   26
3. JKT Mlale             14   7   4   3   13   7   6   25
4. Polisi Tanzania     14   6   6   2   18   12  6   24
5. Mbeya Kwanza      14   6   4   4   14   10  4   22

6. Mufindi                 14   3   4   7   13   21 -8  13

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic