April 1, 2018

Singida United wanakibarua kigumu cha mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga kitakachopigwa Uwanja wa Namfua mjini humo leo.

Kuelekea mechi hiyo inayosubiriwa kwa wingi na mashabiki wa soka mkoani humo na nje ya Singida, wenyeji watakosa huduma ya mchezji wao Danny Usengimana.



Taarifa zilizoandikwa na gazeti la Championi hivi karibuni zilieleza kuwa mchezaji huyo ametimkia kwao Kigali, Rwanda kutokana na madai ya fedha zake za usajili.

Usengimana aliondoka baada ya kuona fedha hizo halipwi na inaelezwa amekuwa akizidai kwa muda mrefu lakini hakuna mafanikio ya kuzipata.

Mbali na Usengimana, Singida pia itakuwa inaendelea kukosa huduma ya mchezaji wake mwingine Daniel Lyanga, ambaye inaelezwa amefungiwa na FIFA kwa muda wa miezi 6 kutokana na kusaini mkataba na timu mbili.

Lyanga inadaiwa alisani mkataba na Singida United wakati akiwa bado ana mkataba na Fanja SC inayoshiriki Ligi Kuu Oman.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic