June 8, 2018







Straika wa Kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta amefunguka kuwa amejipanga vizuri na jeshi lake kuhakikisha wanaibuka na ushindi mkubwa katika mchezo wa kesho dhidi ya Team Kiba.

Samatta anacheza soka la kulipwa katika Klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji ameyasema hayo kuelekea katika mchezo wa kampeni  maalum  iliopewa jina la nifuate kwa ajili ya kuchangia elimu utakaopigwa kesho Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.

 Mshambuliaji huyo amesema kuwa wamejipanga vizuri yeye na timu yake kuhakikisha wanaifunga Team Kiba katika mechi hiyo kutokana na maandalizi waliyoyafanya.

“Tumejiandaa kwa mchezo wa kesho na tupo vizuri chini ya kocha wetu, Julio   na jambo zuri ni kwamba tayari Kiba anajua kwamba tutawafunga mengi.

“Kikubwa ni kuwaomba Watanzania  kujitokeza katika mchezo huo kwa sababu lengo  ni kuchangia elimu ya wadogo zetu, hivyo watu wajitokeze kushuhudia burudani hiyo,” alisema Samatta.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic