BAADA YA KUMSAINI ALIKIBA, COASTAL UNION YATUMA SALAAM HIZI ZA KUTISHA KWA SIMBA NA YANGA
Baada ya kumalizana na nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini Ali Kiba kwa kuingia mkataba wa kuichezea Coastal Union, uongozi wa klabu hiyo umetuma salaam kwa wapinzani wake.
Kupitia Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ndani ya klabu hiyo, Steven Mguto, amesema sasa wapo na moto balaa na wakiahidi kuibuka na ushindi dhidi ya timu zote watakazokutana nazo.
Mguto anaamini kikosi cha Coastal union kitafanya makubwa na kuwashangaza wengi kwa kusema wamefanya usajili maridadi na wapo tayari kwa msimu mpya.
Ikumbukwe Coastal union iliteremka daraja msimu wa 2015/16 pamoja na klabu ya African Sports zote kutoka Tanga lakini sasa wametamba kuwa wanarejea na kishindo kikubwa.







0 COMMENTS:
Post a Comment